VIJANA WANAPASWA KUMTETEA KRISTO
Kwa sababu kila
atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu
atamwonea haya mtu
huyo atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika
watakatifu. Luka
9:26.
Sikuzote umtetee Kristo. Kwa maneno, kwa
roho, na kwa matendo yako, uwe shahidi
wake. Anakupenda, naye anataka kukupa
wewe neema yake nyingi, ili nawe upate
kuwapa wengine.... Kristo amekununua kwa
damu yake mwenyewe. Basi kila mahali,
nyakati zote na chini ya hali zote,
umtetee Yesu. Kumbuka kwamba kwa njia hiyo
utakuwa na mvuto wenye nguvu nyingi sana
juu ya wote unaoshirikiana nao....