JE, NINAMWAKILISHA BWANA WANGU IPASAVYO?
Ninyi ni mashahidi wangu, asema BWANA, na
mtumishi niliyemchagua.( Isaya 43:10).
Iwapo waumini wanafanya urafiki na wale
wasioamini kwa kusudi la kuwaleta kwa Kristo, basi, watakuwa mashahidi wake
Kristo, na baada ya kutekeleza utume wao huo, watajitenga ili kuvuta hewa safi
na takatifu. Wataweza kumkaribia Mungu, na kupeleka dua zao juu kwa Kristo kwa
niaba ya rafiki zao na wale wanaoshirikiana nao, wakijua kwamba anaweza
kuwaokoa kabisa wale wote wamjiao Mungu kwa yeye.
Unapokuwa katika jamii ya wasioamini,
kumbuka daima kwamba kwa tabia yako wewe u mwakilishi wake Yesu Kristo,
usiruhusu maneno ya kipuuzi, na yale yasiyo na maana, yaani, maongezi ya
kipuuzi, kutoka kinywani mwako. Zingatia thamani ya roho ya mtu, nawe kumbuka
kwamba ni haki yako na wajibu wako kwa kila njia inayowezekana kuwa mtenda kazi
pamoja na Mungu. Usijishushe hadhi yako ili upate kuwa sawa na wale wasioamini,
na kucheka na kusema maneno yasiyo na maana kama wao wanavyofanya. Kwa kufanya
hivyo... unajiweka katika hali moja na mwenye dhambi yule. Mwenendo kama huo
utakufanya uwe kikwazo katika njia ya wenye dhambi....