Ijumaa, 4 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

MABWAWA MAKUBWA YA MUNGU 


Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia, Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu. (Zaburi 90:2).

Baba yetu wa Mbinguni ametupatia ishara nyingi zinazoonyesha ukuu wake na utukufu wake. Jambo hilo ni hivyo hasa kwa kiwango cha kustaajabisha katika sehemu hizi za milima....* Mandhari mbalimbali katika milima hii mirefu sana na miinuko yake yenye miamba, makorongo ya milima hii yenye kina kirefu pamoja na vijito vyake vya maji vinavyokwenda kasi na kupiga kelele toka juu ya milima hii, ... maji yake yakipasuka yanapogonga miamba, na kutawanyika katika rasharasha kama mtandio, huifanya mandhari hiyo kuwa nzuri kupita kiasi na yenye utukufu ajabu....

Milima ina hazina zenye mibaraka ambayo Muumbaji amewapa wakazi wa dunia hii. Ni tofauti inayoonekana juu ya uso wa nchi, milimani, katika nyanda tambarare, na mabondeni, ambayo inafunua hekima na uweza wa huyo Mtendakazi Bingwa Mkuu. Na wale ambao wangetaka kuiondolea mbali kutoka katika dunia hii miamba hiyo na milima, makorongo yasiyokaliwa na watu pamoja na vijito vinavyopiga kelele viendavyo kasi, na magenge marefu ----- hao akili zao ... ni finyu mno kuweza kufahamu utukufu wa Mungu ulivyo.

Mungu, Mjenzi Mkuu, ameijenga milima hii mirefu sana, ambayo mvuto wake juu ya hali ya hewa ni mbaraka kwa ulimwengu wetu. Inavuta kutoka mawinguni unyevu mwingi unaourutubisha udongo. Safu za milima ni mabwawa makubwa ya Mungu, yanayoipatia bahari maji yake. Hizo ndizo vyanzo vya chemchemi, vijito, na mito midogo ya maji baridi, pamoja na mito mikubwa. Zinapokea, kwa njia ya mvua na theluji, mvuke uliojaa hewani, na kuusafirisha kwenda chini kwenye nyanda kame, tambarare.

Tungeiangalia milima hiyo isiyokuwa na umbo linganifu kama chemchemi za Mungu zenye mibaraka ambazo kutoka kwazo hububujika maji ya kukidhi mahitaji ya viumbe vyote vilivyo hai. Kila wakati ninapoitazama milima hiyo najisikia moyoni mwangu kujawa na shukrani kwa Mungu.... 

Kila kitu kinachotuzunguka hutufundisha sisi siku kwa siku mafundisho ya upendo wa Baba yetu na ya uweza wake, na ya Sheria zake zinazotawala viumbe vyake vya asili, ambazo ndizo msingi wa serikali zote mbinguni na duniani. ----- MS 62, 1886.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Toa maoni hapa...