Jumatano, 2 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO Jumatano, Septemba 1, 2015

VIUMBE VYA ASILI HUMTANGAZA MUNGU 


Nimezikumbuka siku za kale, Nimeyatafakari matendo yako yote, Naziwaza kazi za mikono yako. Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame. (Zaburi 143:5,6.)

Tumeiangalia milima mirefu sana yenye matuta ya mkingamo katika uzuri wake mkuu, pamoja na buruji zake za miamba zinazofanana na nyumba kubwa za zamani zenye boma [ngome]. Milima hiyo hututangazia sisi ghadhabu ya Mungu iangamizayo ili apate kuithibitisha sheria yake iliyovunjwa; kwa maana [milima hiyo] iliinuliwa juu kwa tetemeko lililoitikisa sana nchi wakati ule wa Gharika. Ni kama mawimbi yenye nguvu nyingi sana yaliyosimama wakati yaliposikia sauti ya Mungu ----- mawimbi yaliyogandishwa, yaliyozuiwa katika kiburi chake kikubwa sana na kuwa mawimbi makubwa. Milima hiyo mirefu sana ni yake Mungu; anakaa juu ya ngome za miamba yake iliyo imara. Utajiri unaotokana na migodi yake ni wake pia, na hivyo ndivyo vilivyo mali yake vilindi vile virefu vya nchi.

Ukitaka kuona ushahidi kwamba Mungu yuko, angalia pande zote po pote bahati yako inapoweza kukuangukia. Anazungumza na fahamu zako na kuugusa moyo wako kwa njia ya kazi zake alizoziumba. Hebu moyo wako na uzipokee picha hizo, ndipo viumbe vya asili vitakuwa kitabu kilichofunguliwa kwako, na vitakufundisha kweli ya Mungu kwa njia ya vitu vya kawaida unavyovifahamu. Miti mirefu sana haitaangaliwa kwa moyo usiojali. Kila ua linalochipua, kila jani lenye mishipa yake myororo, litashuhudia ustadi usio na kifani wa yule Msanii Mkuu sana. Miamba mikubwa sana na milima mirefu sana inayoinuka kule mbali si matokeo ya nasibu. Inatangaza kwa lugha ya kimya inayoshawishi habari za yule Mmoja anayekaa juu ya kiti cha enzi cha malimwengu, yule aliye juu na mwenye kutukuzwa. "Kazi zake zote zajulikana kwa Mungu tangu mwanzo wa ulimwengu." Mipango yake yote ni mikamilifu. Ni kicho na heshima ilioje jina lake lingeweza kuamsha ndani yetu!...

Mungu mwenyewe ndiye Mwamba wetu wa Kale, kimbilio la watu wake, kificho mbali na dhoruba, kivuli jua kali linapounguza. Ametupatia ahadi zake, ambazo ni imara zaidi na madhubuti kuliko miinuko hiyo ya miamba, ni milima ile ya milele. Milima itatoweka, na vilima vitaondolewa; bali fadhili zake hazitaondoshwa, wala agano lake la amani halitaondolewa kwa wale ambao kwa imani wanamfanya yeye kuwa tegemeo lao. Iwapo tungeweza kumtazamia Mungu kutupa msaada wake kwa uthabiti kama ule wa milima hiyo kame yenye miamba, inayozielekea mbingu zilizo juu yake, basi, tusingeweza kuondolewa kamwe katika imani yetu kwake wala katika utii wetu kwa sheria yake takatifu. ---RH, Feb. 24, 1885. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Toa maoni hapa...