Ijumaa, 11 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

MATENDO MEMA HUONGEZEKA KWA KUYAFANYIA MAZOEZI 


Katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu. Tito 2:7, 8.

Mkristo mwenye afya, anayeendelea kukua hatakuwa mpokeaji anayekaa tu bila kutenda lo lote akiwa miongoni mwa wenzake. Yampasa kutoa na vile vile kupokea. Matendo yetu mema huongezeka kwa kuyafanyia mazoezi. Jamii ya Kikristo itatupatia hewa safi ya kuvuta, na katika kuivuta kwetu hatuna budi kuwa na juhudi. Kazi ya Kikristo ifanyike, huruma zetu, kuwatia moyo wengine, na mafundisho vitolewe nasi kwa wale wanaohitaji, kujizuia, upendo, uvumilivu, na ustahimilivu ambavyo huhitajika, vikitumika katika kazi hii ya Kikristo, vitajenga ndani yetu wenyewe imani, utii, tumaini, na upendo kwa Mungu wetu.... Ni jambo la maana ili kuwa na musuli wa kiroho na nguvu kwamba roho iwe na mazoezi. Kazi inapaswa kufanywa kwa utendaji wa kiroho tukizitumia vizuri nafasi za kufanya mema.... Kadiri mtu anavyozidi kuwa mwaminifu katika kufanya kazi zake za Kikristo, ndivyo atakavyozidi kuwa mkamilifu....

Udhaifu na kutokuwa na msimamo wo wote havitatupatia kamwe heshima yo yote katika imani yetu ya Kikristo. Haiwezekani kuwafikia watu kule waliko na kuwainua juu isipokuwa kama tumaini fulani limeamshwa ndani yao kwa njia ya uaminifu na utauwa wako. Huwezi kamwe kuwafikia kwa kushuka chini ya jukwaa hilo la kweli na matengenezo, isipokuwa kwa kuwaleta wengine juu ya jukwaa hilo ambalo Neno la Mungu limekuandalia wewe. Iwapo watu wale wanaoipinga imani yetu wanaona kwamba ninyi mnaoikiri hamna utani, yaani, mko imara, wala hamna tabia mbaya kwa nyakati zote na chini ya hali zote, na ya kwamba mnakaa ndani ya Kristo, Mzabibu hai, na ya kwamba ninyi ni wafuasi wa ile kweli na wafanya matengenezo msioyumba, hapo ndipo mtakapoakisi roho na tabia ile ya Kristo. Katika biashara zenu, katika ushirikiano wenu na waumini pamoja na wale wasio waumini, katika patakatifu [kanisani], nyumbani mwenu, na kila mahali, hapo ndipo mtakapoonyesha mvuto wa upendo wake Mwokozi, ambao utawatawala waumini.

Kipaji, talanta, na fedha sio vya muhimu ili kuweza kuwa na mvuto huo; lakini jambo la maana ni kwamba wewe ukae ndani yake Kristo, maana kwa njia hiyo matunda yako yatakuwa ya haki. ----- Letter 1, 1882.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Toa maoni hapa...