Jumatano, 11 Novemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

CHUNGU CHA MAJARIBU MAKALI YATAKAYOLETA TAABU


Ole! maana siku ile ni kuu, hata hapana inayofanana nayo, maana ni wakati wa taabu yake Yakobo; lakini ataokolewa nayo. Yeremia 30:7.

Njia inayoleta uhuru kutoka dhambini ni ile ya kuisulubisha nafsi, na kupambana na nguvu zile za giza. Na asiwepo mtu ye yote wa kukatishwa tamaa kwa sababu ya maonjo makali watakayokutana nayo katika kipindi kile cha wakati wa taabu ya Yakobo ambacho kiko mbele yao. Wanapaswa kufanya kazi kwa bidii, kwa wasiwasi, si kwa ajili ya wakati ule, bali kwa leo hii. Tunachotaka ni kupata maarifa ya ile kweli kama ilivyo katika Kristo hivi sasa, na kuwa na uzoefu sasa kila mmoja wa kwake [wa maisha yale ya ushindi dhidi ya kila dhambi]. Katika saa hizi za thamani za kufungia mlango wa rehema, tunapaswa kuwa na uzoefu huo wenye kina na ulio hai. Kwa njia hiyo, tutajenga tabia zile zitakazotuhakikishia kuokolewa kwetu katika wakati ule wa taabu.

Wakati wa taabu ni chungu cha majaribu makali ambacho kitazidhihirisha [ndani ya watu wake] tabia zile zinazofanana na ile ya Kristo. Kimekusudiwa kuwaongoza watu wa Mungu wafikie mahali pa kumkataa Shetani na majaribu yake. Pambano lile la mwisho litamfunua kwao Shetani kwa tabia yake halisi, yaani, ile ya mtawala katili anayetumia mabavu, nalo litawafanyia mambo yale ambayo hakuna kitu kingine cho chote ambacho kingeweza kuyafanya, yaani, kumng'oa kabisa [Shetani] kutoka katika mapenzi yao. Kwa maana kuipenda na kuihifadhi dhambi, ni kumpenda na kumhifadhi mwasisi wake, yaani, adui yule wa hatari mno wa Kristo. Wanapotoa udhuru kwa ajili ya dhambi zao na kung'ang'ania tabia ile iliyopotoka, wanampa Shetani nafasi katika mapenzi yao, na kumsujudu. ----- RH, Agosti 12, 1884.

Mbingu yote inampenda mwanadamu na kutaka apate wokovu. Hilo ndilo kusudi kuu katika shughuli yote ya Mungu kwa mtu mmoja mmoja.... Ni jambo linalolishangaza mno jeshi lile la mbinguni kuona kwamba ni wachache mno wanaojali kuwekwa huru kutoka katika utumwa wa mivuto mibaya ya dhambi, wachache sana walio tayari kutumia nguvu zao zote kwa kuafikiana na Kristo katika kazi yake kuu ya ukombozi wao. Kama watu wangeonyeshwa mbele yao picha ya kazi zile anazozifanya yule mlaghai mkuu kwa kuwashikilia wanadamu katika uchungu mkali sana kama ule wa nyongo na kuwaweka katika utumwa ule wa dhambi, ni kwa bidii ilioje wangeyakataa kabisa matendo yale ya giza, ni kwa jinsi gani wangejilinda ili wasianguke majaribuni, wangekuwa waangalifu jinsi gani kuiona na kuiondoa kila kasoro inayoharibu sura ya Mungu ndani yao; kwa jinsi gani wangekaribia sana kando ya Yesu, na kwa jinsi gani dua zao za dhati zingepanda mbinguni ili wapate kutembea kwa amani, karibu zaidi, na kwa furaha na Mungu wao. ----- RH, Agosti 12, 1884.


Jumatano, 21 Oktoba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

JE, NINAMWAKILISHA BWANA WANGU IPASAVYO?


Ninyi ni mashahidi wangu, asema BWANA, na mtumishi niliyemchagua.( Isaya 43:10).

Iwapo waumini wanafanya urafiki na wale wasioamini kwa kusudi la kuwaleta kwa Kristo, basi, watakuwa mashahidi wake Kristo, na baada ya kutekeleza utume wao huo, watajitenga ili kuvuta hewa safi na takatifu. Wataweza kumkaribia Mungu, na kupeleka dua zao juu kwa Kristo kwa niaba ya rafiki zao na wale wanaoshirikiana nao, wakijua kwamba anaweza kuwaokoa kabisa wale wote wamjiao Mungu kwa yeye.

Unapokuwa katika jamii ya wasioamini, kumbuka daima kwamba kwa tabia yako wewe u mwakilishi wake Yesu Kristo, usiruhusu maneno ya kipuuzi, na yale yasiyo na maana, yaani, maongezi ya kipuuzi, kutoka kinywani mwako. Zingatia thamani ya roho ya mtu, nawe kumbuka kwamba ni haki yako na wajibu wako kwa kila njia inayowezekana kuwa mtenda kazi pamoja na Mungu. Usijishushe hadhi yako ili upate kuwa sawa na wale wasioamini, na kucheka na kusema maneno yasiyo na maana kama wao wanavyofanya. Kwa kufanya hivyo... unajiweka katika hali moja na mwenye dhambi yule. Mwenendo kama huo utakufanya uwe kikwazo katika njia ya wenye dhambi....

Ijumaa, 11 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

MATENDO MEMA HUONGEZEKA KWA KUYAFANYIA MAZOEZI 


Katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa kuwa hana neno baya la kunena juu yetu. Tito 2:7, 8.

Mkristo mwenye afya, anayeendelea kukua hatakuwa mpokeaji anayekaa tu bila kutenda lo lote akiwa miongoni mwa wenzake. Yampasa kutoa na vile vile kupokea. Matendo yetu mema huongezeka kwa kuyafanyia mazoezi. Jamii ya Kikristo itatupatia hewa safi ya kuvuta, na katika kuivuta kwetu hatuna budi kuwa na juhudi. Kazi ya Kikristo ifanyike, huruma zetu, kuwatia moyo wengine, na mafundisho vitolewe nasi kwa wale wanaohitaji, kujizuia, upendo, uvumilivu, na ustahimilivu ambavyo huhitajika, vikitumika katika kazi hii ya Kikristo, vitajenga ndani yetu wenyewe imani, utii, tumaini, na upendo kwa Mungu wetu.... Ni jambo la maana ili kuwa na musuli wa kiroho na nguvu kwamba roho iwe na mazoezi. Kazi inapaswa kufanywa kwa utendaji wa kiroho tukizitumia vizuri nafasi za kufanya mema.... Kadiri mtu anavyozidi kuwa mwaminifu katika kufanya kazi zake za Kikristo, ndivyo atakavyozidi kuwa mkamilifu....

Udhaifu na kutokuwa na msimamo wo wote havitatupatia kamwe heshima yo yote katika imani yetu ya Kikristo. Haiwezekani kuwafikia watu kule waliko na kuwainua juu isipokuwa kama tumaini fulani limeamshwa ndani yao kwa njia ya uaminifu na utauwa wako. Huwezi kamwe kuwafikia kwa kushuka chini ya jukwaa hilo la kweli na matengenezo, isipokuwa kwa kuwaleta wengine juu ya jukwaa hilo ambalo Neno la Mungu limekuandalia wewe. Iwapo watu wale wanaoipinga imani yetu wanaona kwamba ninyi mnaoikiri hamna utani, yaani, mko imara, wala hamna tabia mbaya kwa nyakati zote na chini ya hali zote, na ya kwamba mnakaa ndani ya Kristo, Mzabibu hai, na ya kwamba ninyi ni wafuasi wa ile kweli na wafanya matengenezo msioyumba, hapo ndipo mtakapoakisi roho na tabia ile ya Kristo. Katika biashara zenu, katika ushirikiano wenu na waumini pamoja na wale wasio waumini, katika patakatifu [kanisani], nyumbani mwenu, na kila mahali, hapo ndipo mtakapoonyesha mvuto wa upendo wake Mwokozi, ambao utawatawala waumini.

Kipaji, talanta, na fedha sio vya muhimu ili kuweza kuwa na mvuto huo; lakini jambo la maana ni kwamba wewe ukae ndani yake Kristo, maana kwa njia hiyo matunda yako yatakuwa ya haki. ----- Letter 1, 1882.

Alhamisi, 10 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

RAFIKI KWA WALE WASIOKUWA NA RAFIKI 


Marhamu na manukato huufurahisha moyo; Kadhalika utamu wa rafiki ya mtu utokao katika kusudi la moyo wake. Mithali 27:9.

Ingetupasa sisi kuwa na upendo wa Kristo moyoni mwetu kwa kiwango kile ambacho kuwapenda wengine kutakuwa kwa haki na unyofu. Mapenzi yetu yangekuwa na upeo mpana, wala yasingewekwa tu kwa wachache wanaojipendekeza kwetu kwa kutuambia siri zao muhimu. Mwelekeo wa urafiki kama huo ni kutufanya tuwasahau wale walio na hitaji kubwa la kupendwa kuliko wale ambao mawazo yetu yanaelekea kwao.

Jumatano, 9 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

YAKUPASA KUCHAGUA KUNDI LAKO


Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. 2 Wakorintho 6:17.

Mkristo wa kweli hatachagua kundi la wale ambao hawajaongoka. Iwapo Kristo ameumbika ndani, tumaini la utukufu, hatuwezi kufurahia hali ya hewa yenye malaria ya kiroho ambayo inazizunguka roho za wale wanaoipinga dini....

Jumanne, 8 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

CHUNGA MAPENZI YAKO.


Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? 2 Wakorintho 6:14.

Ningependa kukuonya* ujilinde kuhusu ni wapi unayaweka mapenzi yako.... Kumbuka kwamba maisha yako ni mali yake Yesu, na ya kwamba haikupasi kuishi kwa ajili ya nafsi yako tu. Haikupasi kuingia katika uhusiano wa ndoa na mtu asiyekuwa muumini, maana kwa kufanya hivyo, unafanya kinyume kabisa na kile alichoagiza Yesu. Waepuke wale wasioyaheshimu mambo ya dini. Mwepuke yule apendaye kukaa kivivu; mwepuke yule anayeyadhihaki mambo matakatifu. Epuka kushirikiana na yule anayetumia lugha chafu, au mwenye mazoea ya kutumia hata gilasi moja tu ya kileo kikali. Usisikilize posa ya mtu ambaye hautambui wajibu wake kwa Mungu.

Jumatatu, 7 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

UWE NA UWEZO WA KUCHAGUA! 


Wala msishirikiane na matendo yasioyozaa ya giza, bali myakemee. Waefeso 5:11.
Mkristo anapaswa kujitenga mbali na kundi la wale ambao ni kama mtego kwa roho yake. Unapokutana na wale usioweza kuwainua katika hali ile ya hewa iliyo safi na takatifu kwa sababu mwelekeo wao wa kimaadili umepotoka, itakupasa kuwaepuka usishirikiane nao. Watu wa tabaka hiyo kwa kawaida wana utashi wenye nguvu na tabia inayovutia, na yule adui wa Mungu anapowashughulikia, wanakuwa mawakala wake wanaofanikiwa sana katika kuziongoza roho za watu mbali na njia ile ya haki na kwenda katika njia zile za udanganyifu na za hatari. Hali ya hewa ya kimaadili inayowazunguka watu hao imetiwa waa la dhambi, nayo inaleta kwa wengine shinikizo la mvuto unaonajisi. ----- YI, Sept. 29, 1892.

Jumapili, 6 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

HEWA SAFI YA MAADILI 


Ili upate kwenda katika njia ya watu wema, Na kuyashika mapito ya wenye haki. (Mithali 2:20).

Ili kuwa na mwili wenye afya, ni lazima damu izungukayo katika mishipa iwe safi; ili ipate kuwa safi ni lazima ipate hewa safi na chakula safi. Matumizi ya chakula kisichofaa na uvutaji wa hewa chafu huleta ugonjwa ambao hujitokeza katika hali mbalimbali.

Jumamosi, 5 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

HARUFU NZURI KATIKA KAZI YETU YA MAISHA


Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti, nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo. Mathayo 6:28,29.

Msanii wetu Mkuu anayageuza mawazo yetu kuelekea kwenye maua ya mashamba yasiyokuwa na roho, akituonyesha rangi zake nzuri na aina mbalimbali za rangi ambazo ua moja linaweza kuwa nazo. Kwa njia hiyo, Mungu ametufunulia ustadi na utunzaji wake. Hivyo ndivyo ambavyo angelionyesha pendo lake alilo nalo kwa kila mwanadamu. ----- 5BC 1086.

Ijumaa, 4 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

MABWAWA MAKUBWA YA MUNGU 


Kabla haijazaliwa milima, wala hujaiumba dunia, Na tangu milele hata milele ndiwe Mungu. (Zaburi 90:2).

Baba yetu wa Mbinguni ametupatia ishara nyingi zinazoonyesha ukuu wake na utukufu wake. Jambo hilo ni hivyo hasa kwa kiwango cha kustaajabisha katika sehemu hizi za milima....* Mandhari mbalimbali katika milima hii mirefu sana na miinuko yake yenye miamba, makorongo ya milima hii yenye kina kirefu pamoja na vijito vyake vya maji vinavyokwenda kasi na kupiga kelele toka juu ya milima hii, ... maji yake yakipasuka yanapogonga miamba, na kutawanyika katika rasharasha kama mtandio, huifanya mandhari hiyo kuwa nzuri kupita kiasi na yenye utukufu ajabu....

Alhamisi, 3 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO Alhamisi, Septemba 3, 2015

SHULE YA AKILI NA MAADILI 


Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa. (Ufunuo 15:3.)

Mwasisi Mkuu ameumba na kuzitengeneza mandhari mbalimbali katika maumbile [ulimwengu huu] ili zipate kuwa na maana kubwa katika tabia ya mwanadamu kiakili na kimaadili. Hizo zinatakiwa ziwe shule ya Mungu ya kuikuza akili na maadili. Hapo ndipo akili inaweza kuwa na nyanja pana sana ya utafiti katika maonyesho hayo ya matendo makuu ya Mungu wa milele. Miamba ni miongoni mwa vitu vya thamani ulimwenguni, ikiwa na hazina za hekima na maarifa. Katika miamba na milima hiyo umeandikwa ukweli kwamba hakika Mungu aliwaangamiza kwa Gharika wale waovu juu ya uso wa nchi hii. ----- MS 73, 1886.

Jumatano, 2 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO Jumatano, Septemba 1, 2015

VIUMBE VYA ASILI HUMTANGAZA MUNGU 


Nimezikumbuka siku za kale, Nimeyatafakari matendo yako yote, Naziwaza kazi za mikono yako. Nakunyoshea mikono yangu; Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame. (Zaburi 143:5,6.)

Tumeiangalia milima mirefu sana yenye matuta ya mkingamo katika uzuri wake mkuu, pamoja na buruji zake za miamba zinazofanana na nyumba kubwa za zamani zenye boma [ngome]. Milima hiyo hututangazia sisi ghadhabu ya Mungu iangamizayo ili apate kuithibitisha sheria yake iliyovunjwa; kwa maana [milima hiyo] iliinuliwa juu kwa tetemeko lililoitikisa sana nchi wakati ule wa Gharika. Ni kama mawimbi yenye nguvu nyingi sana yaliyosimama wakati yaliposikia sauti ya Mungu ----- mawimbi yaliyogandishwa, yaliyozuiwa katika kiburi chake kikubwa sana na kuwa mawimbi makubwa. Milima hiyo mirefu sana ni yake Mungu; anakaa juu ya ngome za miamba yake iliyo imara. Utajiri unaotokana na migodi yake ni wake pia, na hivyo ndivyo vilivyo mali yake vilindi vile virefu vya nchi.

Jumapili, 30 Agosti 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO Jumapili, Agosti 30, 2015

VIJANA WANAPASWA KUMTETEA KRISTO

Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu
atamwonea haya mtu huyo atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika
watakatifu. Luka 9:26.

Sikuzote umtetee Kristo. Kwa maneno, kwa roho, na kwa matendo yako, uwe shahidi
wake. Anakupenda, naye anataka kukupa wewe neema yake nyingi, ili nawe upate
kuwapa wengine.... Kristo amekununua kwa damu yake mwenyewe. Basi kila mahali,
nyakati zote na chini ya hali zote, umtetee Yesu. Kumbuka kwamba kwa njia hiyo
utakuwa na mvuto wenye nguvu nyingi sana juu ya wote unaoshirikiana nao....

Jumanne, 25 Agosti 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO Jumanne, Agosti 25, 2015

CHUNGA HATUA YAKO! 

  
 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike. Mithali 4:26.

"Mkaifanyie miguu yenu njia za kunyoka," asema mtume, "ili kitu kilicho kiwete kisipotoshwe." Waebrania 12:13. Njia ile inayokwenda mbali na Mungu, yaani, mbali na kanuni yake ya haki, takatifu, na kamilifu [Amri Kumi], sikuzote imepotoka na ni ya hatari. Hata hivyo... wengi wamekuwa wakienda katika njia hiyo ya uasi. Katika mifano mingi [inayofahamika], hawakuanza vizuri katika utoto na ujana wao, nao wamezifuata njia hizo potofu katika safari yao yote. Sio tu kwamba wao wenyewe wamekosa kwa kuiacha njia ile ya kweli, bali kwa mvuto wa mfano wao wengine vile vile wamepotoshwa kutoka katika njia ile dhahiri iliyonyoka, nao wamefanya makosa ya kufisha....

Jumapili, 26 Julai 2015

LESONI LEO:-“UHAMISHO" -Jumapili, Julai 26, 2015


Soma Isaya 39:5-7 na Danieli 1:1,2. Je, aya hizi zinahusianaje?
Danieli, ambaye jina lake humaanisha “Mungu ni hakimu wangu” alilazimishwa kutembea toka Yerusalemu, mji uliokuwa umeshindwa, hadi katika mji mkuu wa Babeli. Kitabu cha Danieli hutoa picha kidogo ya maisha yake katika ikulu za Babeli na Uajemi. Baada ya miaka mitatu ya “elimu” huko Babeli, Danieli aliajiriwa kama mtumishi wa serikali na mshauri wa mfalme. Kupitia uweza wa Mungu, alipanda juu kuliko hadhi ya kawaida ya mateka na kuwa mmisionari mstahiki katika yale mataifa makubwa mawili.

USOMAJI WA BIBLIA LEO:- MWANZO 15- Jumapili, Julai 26, 2015

Mwanzo 15

1 Baada ya mambo hayo neno la Bwana likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako kubwa sana.

2 Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini, nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu Eliezeri, Mdameski?

Jumamosi, 25 Julai 2015

IBADA YA SABATO YA LEO, Julai 25, 2015: - "MUNGU AMETUCHAGUA TUFANYWE WATOTO WAKE" - hubiri kutoka kwa Mchungaji Amos Lutebekela

WIMBO: Namba  142- NASIKIA MWITO

FUNGU KUU:,"kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo. 5Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake." ( Waefeso 1:4 - 5)
UFAFANUZI:
Ni Mungu anayetuchagua na kutupatia uwezo wa kufanya kila jambo, hata tendo hili la kuingia kanisani katika sabato ya leo ni Mungu ndiyo amechagua, na hili hutokea mara tu pale tunapokubali uchaguzi huu uliotoka kwa Mungu yaani kuchaguliwa kuwa watoto wa Mungu.

LESONI 5:- WAMISIONARI UHAMISHONI - Julai 25 - 31, 2015

Sabato Mchana

Somo la Juma Hili: Danieli 1-12; Isaya 39:5-7; Danieli 2:44; Mathayo 24:14,15; Mwanzo 41.
Fungu la Kukariri: “‘Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa. ’” (Danieli 7:14).

Kama watu wa unabii, Waadventista wa Sabato huamini katika kurudi upesi kwa Yesu Kristo. Kuja kwake kutaifikisha dunia hii katika mwisho wake, na kuanzisha zama mpya ya ufalme wa milele wa Mungu, kama ilivyoelezwa ifuatavyo katika kitabu cha Danieli: “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii” (Dan. 7:27). Ufalme huu ndivyo utimilifu wa imani yetu; ni kile ambacho kitabu cha Waebrania (Ebr. 11:16) inakiita “nchi iliyo bora”, ambayo watu wote wa Mungu wa vizazi vyote waliisubiria kwa hamu, ambayo “mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu” (Waebrania 11:10).

Lakini kitabu cha Danieli pia ni kama mwongozo wa shughuli za umisionari. Katika kitabu hicho tunaweza kupata masomo kuhusu namna Mungu alivyoweza kuwatumia baadhi ya watu kushuhudia kwa wale waliokuwa katika ujinga wa kiroho na kiteolojia. Kupitia uaminifu wao na bidii yao, na imani thabiti, waumini hawa waliudhihirisha ukweli wa Mungu aliye hai kwa wale waliojua tu miungu ya uongo, na hivyo wakawapatia wale wapangani nao fursa ya kuwa na nafasi katika ufalme wa milele.

USOMAJI WA BIBLIA LEO- MWANZO 14 - Jumamosi , Julai 25, 2015


Mwanzo 14

1 Ikawa siku za Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, na Kedorlaoma mfalme wa Elamu na Tidali mfalme wa Goimu,

2 walifanya vita na Bera mfalme wa Sodoma na Birsha mfalme wa Gomora, na Shinabu mfalme wa Adma, na Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari.

3 Hawa wote wakakutana panapo bonde la Sidimu, kwenye Bahari ya Chumvi.

4 Miaka kumi na miwili walimtumikia Kedorlaoma, hata mwaka wa kumi na tatu wakaasi.

5 Na mwaka wa kumi na nne akaja Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja naye, wakawapiga Warefai katika Ashteroth-karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, na Waemi katika Shawe-kiryathaimu,

Ijumaa, 24 Julai 2015

USOMAJI BIBLIA LEO:- MWANZO 13 - Ijumaa, Julai 24, 2015

Mwanzo 13

Abramu akapanda kutoka Misri, yeye, na mkewe, na kila alichokuwa nacho, na Lutu pamoja naye, mpaka kusini.

2 Naye Abramu alikuwa ni tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha, na kwa dhahabu.

Alhamisi, 23 Julai 2015

USOMAJI WA BIBLIA LEO: - MWANZO 12 - Alhamisi, Julai 23, 2015

Mwanzo 12

Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

LESONI YA ALHAMISI:- KILIO CHA NINAWI - Julai 23, 2015


Yona 4:1-11 huthibitisha kuwa kikwazo kikubwa kwa Mungu kumfanya nabii wake ahusike katika utume kwa ulimwengu hakikuwa umbali, upepo, mabaharia, samaki, au watu wa Ninawi.

KESHA LA ASUBUHI:- UKUTA WA MOTO DHIDI YA MAJARIBU - Alhamisi, Julai 23, 2015

Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi. Zaburi 119:11.
Shetani anatafuta daima kuishawishi mioyo ya wanadamu kwa hila zake.
Yeye ndiye mwanzilishi mwamba; alipewa uwezo huo na Mungu, lakini akauharibu uwezo wake wote mtukufu kwa kuyapinga na kuyafanya mashauri yake yule Aliye juu sana yasiwe na maana yo yote....

Jumatano, 22 Julai 2015

LESONI JUMATANO, Julai 22, 2015- KIZAZI CHA NINAWI


Somo Yona 3. Ni ujumbe gani muhimu unapatikana hapa katika muktadha wa kushuhudia na uinjilisti?

"Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili,kusema, Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa; ukaihubiri habari nitakayokuamuru." (Yona 3:1,2).

USOMAJI WA BIBLIA LEO Jumatano, Julai 22, 2015


Mwanzo 11

1 Nchi yote ilikuwa na lugha moja na usemi mmoja.

2 Ikawa watu waliposafiri pande za mashariki waliona nchi tambarare katika nchi ya Shinari; wakakaa huko.

3 Wakaambiana, Haya, na tufanye matofali tukayachome moto. Walikuwa na matofali badala ya mawe, na lami badala ya chokaa.

KESHA LA ASUBUHI: MKATE UNAOSHIBISHA - Jumatano, Julai 22, 2015

Mimi ndimi chakula [mkate] chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. 
Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.... 

Jumanne, 21 Julai 2015

KESHA LA ASUBUHI: Jumanne, Julai 21, 2015-MAJANI YA MTI ULE WA UZIMA

Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; 
yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.
" Yohana 6:35. Ulimwengu unaangamia kwa kuikosa kweli, kweli ile safi, isiyoghoshiwa. Kristo ndiye ile kweli. Maneno yake ndiyo kweli. ----- MS 130, 1897.

USOMAJI WA BIBLIA LEO Jumanne, Julai 21, 2026

Mwanzo 9

1 Mungu akambariki Nuhu na wanawe, akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi.

2 Kila mnyama wa katika nchi atawaogopa ninyi na kuwahofu, na kila ndege wa angani: pamoja na vitu vyote vilivyojaa katika ardhi, na samaki wote wa baharini; vimetiwa mikononi mwenu.

Jumatatu, 20 Julai 2015

LESONI YA LEO JUMATATU Julai 20, 2015: Mmisionari wa Awali


"Ondoka, uende Ninawi!" lilikuwa ndilo agizo la Mungu kwa Yona. Katika Agano la Kale wito jwa kawaida ulikuwa "Njoni Sayuni." Mpango wa Mungu wa awali ulikuwa kwamba Isaeli wapate kuishi kivitendo kulingana na dini yao, kiasi cha kuwafanya Mataifa mengine wavutwe kuja kwao kutafuta ushauri (Isaya 56:70).

USOMAJI WA BIBLIA LEO Jumatatu, Julai 20, 2015.


Mwanzo 8

1 Na Mungu akamkumbuka Nuhu, na kila kilicho hai, na wanyama wote waliokuwamo pamoja naye katika safina; Mungu akavumisha upepo juu ya nchi, maji yakapungua;

Jumapili, 19 Julai 2015

USOMAJI WA BIBLIA LEO Jumapili, Julai 19, 2015

Mwanzo 7
1 Bwana akamwambia Nuhu, Ingia wewe na jamaa yako yote katika safina; kwa maana nimekuona wewe u mwenye haki mbele zangu katika kizazi hiki.

LESONI 4 : KISA CHA YOHANA, Julai 18-24, 2015

SABATO MCHANA
Sabato Mchana
Somo la Juma Hili: Yona 1-4; 2 Wafalme 14:25; Isaya 56:7; Isaya 44:8; Mathayo 12:40; Ufunuo 14:6-12.

Fungu la Kukariri: “‘Hakika natambua ya kuwa Mungu hana upendeleo; bali katika kila mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yete’” (Matendo 10:34, 35).

Kisa cha Yona ni maelezo kuhusu nabii Mwebrania aliyekuwa akihudumu nje ya eneo alilokuwa analipenda.

Jumamosi, 18 Julai 2015

USOMAJI WA BIBLIA LEO Jumamosi, Julai 18, 2015

Mwanzo 6
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

HABARI PICHA KATIKA IBADA YA LEO SINZA SDA CHURCH

Mtumishi wa Mungu Ashery Anthony  akinena na waumini waliohudhuria ibada ya Sinza leo

Kwaya ya kanisa la Sinza Sauti Ya Nyikani ikimtukuza Mungu katika ibada ya leo 


WATATU WAMEJITOA KIKAMILIFU KWA AJILI YA UBATIZO KATIKA IBADA YA LEO ILIYOENDESHWA NA MZEE WA KANISA Mr. Ashery Anthony

Wa kwanza kutoka kulia ni Karani wa kanisa Mr. Joseph Kengera akiandikisha majina ya makamanda hao wa Yesu walijitoa kwa ubatizo katika ibada ya leo.
Ikiwa ni katika kutokuionea aya imani juu ya Yesu Kristo, vijana watatu leo wamemkataa shetani mbele ya washiriki wa kanisa la Sinza kwa kuamua kujitoa kikamilifu kwa ajili ya ubatizo wa maji mengi kupitia kanisa la waadventista wa Sabato Sinza.

SABATO YA LEO Julai 18, 2015: "TABIBU WA KWELI WA DHAMBI" hubiri kutoka kwa Mzee Ashery Anthony


WIMBO: Namba  111- TABIBU MKUU

FUNGU KUU:,"Na  kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi , atasamehewa. Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye  haki kwafaa sana akiomba kwa bidii." ( Yakobo 5:15 -16)
Mzee wa Kanisa Ashery Anthony akihubiri katika ibada ya leo

Jumanne, 14 Julai 2015

KESHA LA ASUBUHI: HIVI NI KWELI TUNAJITOLEA MHANGA? Jumanne, Julai 14, 2015

Washangilie,wakufurahie, Wote wakutafutao.

Waupendao wokovu wako waseme daima, Atukuzwe BWANA. Zaburi 40:16. Wengi wanasema juu ya maisha ya Mkristo kuwa yanatuondolea anasa na raha za dunia.

Mimi nasema hayaondoi kitu chochote kinachofaa kukitunza. Je, kuna mashaka, umaskini, na dhiki anayopata Mkristo? Ndiyo, jambo hilo linatazamiwa katika maisha haya.

Jumatatu, 13 Julai 2015

KESHA LA ASUBUHI: KIPIMO CHA TABIA - Jumatatu, Julai 13, 2015

Lakini  hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana  na imani, na kujichoma kwa maumivu mengi. 1 Timotheo 6:9,10.

Jumamosi, 11 Julai 2015

"USHINDI WA KURA YA HAPANA DHIDI YA KUWEKEWA MIKONO YA WAKFU WANAWAKE HAIBADILI SERA YA SASA YA KANISA" alisema Rais Ted Wilson

Divisheni ya Amerika ya kaskazini inasema itaendelea kuhamasisha wanawake kutumika katika huduma ya injili.

Rais wa Baraza kuu Ted N.C. Wilson alisema hapo jana kwamba kura iliyopigwa wiki hii kuhusu suala la kuwawekea mikono ya wakfu wanawake ilimaanisha “tumedumisha sera ya sasa.”

Alhamisi, 9 Julai 2015

MAREKEBISHO YA KIHISTORIA YA IMANI 28 ZA MSINGI ILI KUENDANA NA WAKATI WA SASA YAPITISHWA NA WAJUMBE WA MKUTANO MKUU 2015

Wajumbe wapitisha mabadiliko ya kihistoria ya Imani za Msingi za Kanisa la Waadventista wa Sabato
Ezekiel Adeleye, kutoka Divisheni ya Africa Magharibi ya kati , akipiga kura kupitisha Imani ya Msingi namba 1 kuhusu Maandiko matakatifu.
Marekebisho hayo yamefanyika ili kuendana na wakati wa sasa pamoja na kuimarisha uandishi wa imani hizo ili kueleweka kwa urahisi pasipo kubadili dhana kuu ya kila imani ya msingi.
Tangun ilipopitishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1980, Imani za Msingi zilikuwa hazijawahi kupitiwa upya tena ukiacha ile imani moja ya ziada iliyopitishwa mwaka 2005.

Hivyo idhini ya wajumbe wa Mkutano Mkuu siku ya jumanne, julai 7, 2015 kupitia upya tena Imani hizo ilikuwa ni hitimisho la mchakato wa miaka mitano ya upitiaji na uboreshaji upya wa Imani za Msingi za Kanisa la Waadventista wa Sabato.

HOJA YA KUWEKEWA MIKONO YA WAKFU WANAWAKE HAIJAPITISHWA

"Hakuna ushindi juu ya jambo hili," alisema MICHAEL L. RYAN. "Hakuna washindi wala walioshindwa."

Roho Mtakatifu ameongoza wajumbe wa kikao cha General Conference 2015 kupiga kura ya HAPANA, kuhusu suala la kuwawekea mikono ya wakfu kwa kazi takatifu wanawake.

Kwa kiasi cha kura 1381 za ndiyo, 977 za hapana, na 5 ambazo hazikupigwa, wajumbe kwa kura ya siri walimaliza mchakato wa miaka mitano kuhusu kwawekea mikono wanawake uliotawaliwa kwa majadiliano mazito na wakati mwingine kutumika hata kwa lugha kali za kuudhi.

Jumatano, 8 Julai 2015

TAARIFA YA MHAZINI MKUU KATIKA KIKAO CHA GC 2015, July 05, 2015 | San Antonio, Texas, United States of America | Robert Lemon

ROBERT LEMON
MHAZINI WA GENERAL CONFERENCE
Robert Lemon, Mhazini anayemaliza muda wake, aliwasilisha Taarifa ya Mhazini kwa mwaka 2015 mnamo siku ya Ijumaa, Julai 3.

ZAKA NA SADAKA


Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, zaka ya kila mwaka duniani kote imeongezeka kwa 31% kutoka dola za kimarekani bilioni 1.85 mwaka 2009 hadi dola za kimarekani bilioni 2.43 mwaka 2014.

USOMAJI WA BIBLIA LEO Alhamisi, Julai 8, 2015

Ufunuo 17

Kahaba Mkuu na Mnyama

1 Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;2ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.

MCHUNGAJI GEOFREY MBWANA ACHAGULIWA TENA KUWA MAKAMU WA RAISI WA GENERAL CONFERENCE

Pr. Geoffrey Mbwana
Makamu wa Raisi wa General Conference 2015-2020







Jumanne, 7 Julai 2015

MSHIRIKI WA KANISA LA USHINDI SDA ACHAGULIWA KUWA MJUMBE WA BODI YA UKAGUZI YA GENERAL CONFERENCE 2015 - 2020

 
ESTHER ABAYO
MSHIRIKI WA KANISA LA USHINDI SDA, DAR ES SALAAM , TANZANIA
Esther Abayo ambaye ni mshirirki wa kanisa la Waadventista wa Sabato Ushindi Dar-es-Salaam, Tanzania amechaguliwa kuwa Mjumbe wa Bodi ya Ukaguzi ya General Conference (GCAS) 2015-2020, katika kikao cha Baraza Kuu la Kanisa la Waadventista wa Sabato Ulimwenguni (General Conference Session ) 2015.

USOMAJI WA BIBLIA LEO

JUMANNE, JULAI 7 , 2015

Ufunuo 15

Malaika Saba wenye Mapigo Saba ya Mwisho

1 Kisha nikaona ishara nyingine katika mbingu, iliyo kubwa, na ya ajabu; malaika saba wenye mapigo saba ya mwisho; maana katika hayo ghadhabu ya Mungu imetimia.

KESHA LA ASUBUHI

NI LAANA AU MBARAKA?

Msijiwekee hazina duniani, nondo na kutu viharibupo, na wevi huvunja na kuiba.
Mathayo 6:19. 
Hazina ni vitu vile vinavyoujaza sana moyo, na kuchota mawazo yote, na kumwacha nje Mungu na ile kweli.

Jumatatu, 6 Julai 2015

Mchungaji Bina Afungua Rasmi Mkutano wa TAiN-Tanzania Adventist Internet Network, 2015

Monday, June 22, 2015


MOTTO: TAIN 2015, UBUNIFU ZAIDI.

Mafundi mitambo wakiweka mambo sawa tayari kwa kuanza Mkutano.
Mchungaji HARUNI KIKIWA akiwa anaongoza Uimbaji katika Mkutano.
Somo la Ufunguzi wa mkutano wa TAIN 2015, limetolewa na Mch. Bina kutoka ECD likijengwa kutoka katika kitabu cha Mathayo 24. Aidha amesisitiza viongozi wa Tehama kuwa makini kwani hizi ni siku za mwisho.
"Bwana atakomesha maisha yetu siku moja na hivyo tunapaswa kutengeneza maisha yetu na sio kujiinua kwa mafanikio yetu" Amesema Mch. Bina

MBARAKA WA MASTER GUIDE 2 WAPYA NDANI YA KANISA LA WAADVENTISTA WA SABATO SINZA


Master Guide Rebecca
Master Guide Malekela
Miongoni mwa makanisa yaliyofanikiwa kuhitimisha Master Guide mafunzoni katika kambi la mafunzo kwa vijana huko Chimala, Mbeya ni Kanisa la Sinza SDA kutoka Dar es Salaam.

MATUKIO KATIKA PICHA YA KAMBI LA CHIMALA, MBEYA JUNI 21 - 28, 2015

Master Guide Kelvin Peter(Aliyevaa Uniform) akipata chai na Vijana wa kambi
Balozi Neria, Neema, na Suzy kutoka kanisa la Sinza pamoja na AY Mariamu wakifuatilia mafunzo kwa makini

Jumamosi, 4 Julai 2015

ALICHOSEMA TED N.C. WILSON MUDA MFUPI MARA BAADA YA KUCHAGULIWA KUWA RAISI TENA

“Hakuna anayeweza kushughulikia nafasi hii isipokuwa kwa kuongozwa moja kwa moja  na Uongozi wa Mungu.Hivyo ni uzoefu wa kujishusha sana."

WAJUMBE WA KIKAO CHA GC, 2015 WATUMIA MFUMO MPYA WA KIELECTRONIC KUPIGA KURA

BOFYA HAPA KUONA VIDEO
Mchungaji Dr. Blasiusc Luguri akisifia mfumo mpya wa kielectronic uliotumika katika kuchagua viongozi wa GC mwaka huu 2015.

YALIYOJILI SIKU YA PILI KATIKA KIKAO CHA GENERAL CONFERENCE

UNION CONFERENCE MPYA 35 ZAPITISHWA KATIKA KIKAO CHA GC 2015

Ted N.C. Wilson akihutubia wajumbe wa kikao cha Mkutano Mkuu siku ya kwanza ya kikao.

TED N.C. WILSON ACHAGULIWA TENA KUWA RAIS WA WAADVENTISTA WASABATO ULIMWENGUNI

Ted N.C. Wilson speaks to delegates shortly after his reelection as General Conference president. [Photo ©2015 Adventist Review / ANN. Photos by Josef Kissinger]

WILSON ACCEPTS THE NEW FIVE-YEAR TERM WITH “QUIET RESPECT AND HUMILITY.”

Delegates overwhelming elected incumbent General Conference president Ted N.C. Wilson to another five years in office on Friday.
An estimated 90 percent of some 1,900 registered delegates voted in favor of continuing Wilson in his position as leader of the Seventh-day Adventist world church after a 37-minute discussion at the General Conference session in San Antonio, Texas.

SIKU YA UFUNGUZI, GC SESSION 2015

USOMAJI WA BIBLIA LEO

Ufunuo 9

1Kisha, malaika wa tano akapiga tarumbeta yake. Nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka juu ya nchi kutoka mbinguni. Nayo ikapewa ufunguo wa shimo la kuzimu. 2Basi, nyota hiyo ikafungua shimo la kuzimu, kukatoka moshi wa tanuri kubwa. Jua na anga vikatiwa giza kwa moshi huo wa kuzimu. 3Nzige wakatoka katika moshi huo, wakaingia duniani, wakapewa nguvu kama ya nge.