Jumatatu, 7 Septemba 2015

SOMO LA ASUBUHI LEO

UWE NA UWEZO WA KUCHAGUA! 


Wala msishirikiane na matendo yasioyozaa ya giza, bali myakemee. Waefeso 5:11.
Mkristo anapaswa kujitenga mbali na kundi la wale ambao ni kama mtego kwa roho yake. Unapokutana na wale usioweza kuwainua katika hali ile ya hewa iliyo safi na takatifu kwa sababu mwelekeo wao wa kimaadili umepotoka, itakupasa kuwaepuka usishirikiane nao. Watu wa tabaka hiyo kwa kawaida wana utashi wenye nguvu na tabia inayovutia, na yule adui wa Mungu anapowashughulikia, wanakuwa mawakala wake wanaofanikiwa sana katika kuziongoza roho za watu mbali na njia ile ya haki na kwenda katika njia zile za udanganyifu na za hatari. Hali ya hewa ya kimaadili inayowazunguka watu hao imetiwa waa la dhambi, nayo inaleta kwa wengine shinikizo la mvuto unaonajisi. ----- YI, Sept. 29, 1892.

Marafiki zako unaoshirikiana nao hawawezi kutazamiwa kuwa huru mbali na upungufu mwingi katika tabia zao au dhambi. Lakini katika kuchagua marafiki zako, ungeweka kipimo chako juu sana kadiri unavyoweza. Namna ya maadili yako yalivyo hupimwa kwa aina ya marafiki unaowachagua. Epukana na kufanya urafiki wa karibu sana na wale ambao mfano wao usingechagua kuuiga....

Chagua kuwa marafiki zako wale ambao wanaiheshimu sana dini na kuyaweka katika matendo yao maongozi yake. Daima weka mbele yako maisha yale ya baadaye. Marafiki zako wasiondoe mawazo hayo moyoni mwako. Hakuna kitu kitakachofukuzilia mbali mawazo hayo ya maana kama kuongea na watu wa ovyo, yaani, wale wasioijali, wala kuipenda dini. Haidhuru wawe wamefikia kisomo cha juu jinsi gani, kama hawaiheshimu dini, au hawaijali, basi, hao wasingekuwa marafiki zako wateule. Kadiri tabia zao zinavyovutia kwa njia zingine, ndivyo kadiri ungeweza kuuogopa mvuto wao kama wenzi wako, kwa sababu wangekuzungushia mvuto wao usiokuwa wa kidini, wa kikafiri, yaani, usioheshimu mambo matakatifu, na hata hivyo wanaweza kuuchanganya na mambo yao mengi ya kuvutia kiasi kwamba itakuwa ni hatari kweli kwa maadili yako. ---- Letter 17, 1878.

Uwe shujaa kama Danieli. Uwe shujaa kusimama peke yako.... Ukimya unaoletwa na woga mbele ya marafiki zako waovu, wakati wewe unasikiliza hila zao, hukufanya wewe kuwa mmoja wao.... Uwe na ujasiri kutenda mema. ----- 3BC 1155.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Toa maoni hapa...