Alhamisi, 9 Julai 2015

HOJA YA KUWEKEWA MIKONO YA WAKFU WANAWAKE HAIJAPITISHWA

"Hakuna ushindi juu ya jambo hili," alisema MICHAEL L. RYAN. "Hakuna washindi wala walioshindwa."

Roho Mtakatifu ameongoza wajumbe wa kikao cha General Conference 2015 kupiga kura ya HAPANA, kuhusu suala la kuwawekea mikono ya wakfu kwa kazi takatifu wanawake.

Kwa kiasi cha kura 1381 za ndiyo, 977 za hapana, na 5 ambazo hazikupigwa, wajumbe kwa kura ya siri walimaliza mchakato wa miaka mitano kuhusu kwawekea mikono wanawake uliotawaliwa kwa majadiliano mazito na wakati mwingine kutumika hata kwa lugha kali za kuudhi.
Wajumbe wameizima kabisa hoja ambayo ingeliruhusu kila divisheni ya Kanisa la wa Sabato kuamua wenyewe kuwawekea mikono ya wakfu kwa kazi takatifu wanawake kwenye huduma ya injili katika maeneo yao.

Rais wa Baraza kuu la Kanisa ulimwenguni Teddy N.C Wilson akihutubia wajumbe mara baada ya matokeo ya kura kutangazwa katika kikao cha Baraza kuu mwaka 2015 huko San Antonio, Texas, Marekaniametoa wito kwa washiriki wa kanisa duniani kote kuungana katika utume wa kanisa."Sasa ni wakati wa kuungana chini ya bendera ya damu ya Yesu Kristo na nguvu zake, si nguvu zetu," Wilson alisema ha uwanja Alamodome. "Sasa ni wakati wa kuunganisha katika dhamira yetu kama kanisa la Kristo."               
Rosa T Banks akiwasomea  wajumbe wa baraza  swali wanalopaswa kulipigia kura muda mchache baadae  mara baada ya ombi maalumu kuombea zoezi hilo kutolewa.

Swali lililopigiwa kura:
Baada ya utafiti wako kwa nja ya maombi katika biblia, maandishi ya Ellen G.White, na taarifa ya tume ya utafiti juu ya kuwekewa mikono ya wakfu kwa kazi takatifu, na;
Baada ya kuzingatia kwako kwa umakini kwamba kipi ni bora kwa ajili ya kanisa na utimilifu wa lengo lake.
Inakubalika kwa kamati ya utendaji ya divisheni kwa namna wanavyoweza kudhani ni sahihi kulingana na maeneo yao, kuwa na vifungu vya kuwekea mikono ya wakfu wanawake kwa kazi takatifu kwenye huduma ya injili? Ndiyo au Hapana
i.e
After your prayerful study on ordination from the bible, the writing of Ellen G. White, and the reports of the study commissions, and;
After your careful consideration of what is best for the church and the fulfillment of its mission,
It is acceptable for division executive commitees as they may deem it appropriate in their territories, to make provision for the ordination of women to the gospel ministry? Yes or No
At the conclusion of the vote the count was as follows:
  • No: 1381
  • Yes: 977
  • Abstain: 5
  • Total: 2363
Jibu: 
Hitimisho la kura ziliohesabiwa ilikuwa kama ifuatavyo, waliosema:
  • Ndiyo ni 977 sawa na 41% ya waliopiga kura.
  • Hapana ni 1381 sawa na 58% ya waliopiga kura.
  • Wasiopiga kura ni 5.
  • Jumla ya kura zote ni 2363.
Michael L. Ryan, Makamu wa Rais wa GC  mtaafu ambaye ndiyo alikuwa mwenyekiti wa majadiliano akiomba ombi maalumu la kuhitimisha maombi ya wajumbe wote waliokuwa wakiomba  kwa ajili ya zoezi la upigaji kura  ili kuamua kama ni Ndiyo au Hapana.
MAELEKEZO KABLA YA KUPIGA KURA
Myron akitoa maelekezo yaliyopaswa kuzingatiwa na wajumbe ili kufanikisha zoezi la upigaji kura
Maelekezo yameendelea kutolewa kama yanavyoonekana katika picha
ZOEZI LA KUPIGA KURA LIMEANZA
Wajumbe wakiendelea na zoezi la kupiga kura mara baada ya maelekezo kukamilika



ZOEZI LA KUHESABU KURA LIKIENDELEA 
Wajumbe wakidumu kuimba mara baada ya kumaliza kupiga kura huku wakisubiri zoezi la kuhesabu kura likamilike
Zoezi la kuhesabu kura likiendelea

MATOKEO, Roho Mtakatifu ameongoza kwenye kura ya hapana. Hakuna kuwekea mikono wanawake, Tuombee umoja na tuangalie kazi tuliyotumwa.

Jumla ya wajumbe 40 - 20 wanaounga mkono hoja na 20 wanaopinga hoja - walichukua vipaza sauti kueleza msimamo wao kuhusu hoja. Mjadala ulisimamishwa mara 35, kwa vitendo vya wajumbe kuomba mwongozo kuhusu utaratibu, pingamizi kwa namna baadhi ya mambo yalivyokuwa yakichukuliwa.

Pia Ryan mwenyekiti wa mjadala alimwalika Jan Paulsen, Rais Mstaafu wa Baraza Kuu (General Conference), kuongea.

Paulsen alisihi wajumbe wapige kura ya “ndiyo,” alisema lilikuwa ni suala la uaminifu. Alisema washiriki wa kanisa walipaswa kuamini kwamba wenzao katika divisheni zingine walijua vizuri ni nini makanisa yao mahalia wanahitaji.

Ryan pia alimwalika Teddy N.C. Wilson kuongea. Wilson hakuwa na pendekezo la kupiga kura ya “ndiyo” au “hapana” , akisema tu, “Maoni yangu kwa kiwango fulani yanajulikana na ninaamini yamejengwa katika msingi wa kibiblia.”

“Tumejaribu kuwa na uwazi, uaminifu na umakini, na kuhakikisha usiri wa kura kwa kadri ya uwezo wetu," alisema Nancy Lamoreaux, Afisa Habari Mkuu wa General Conference na mratibu wa vitendea kazi kwa ajili ya kupiga kura.

Rais Teddy Wilson alifungua kikao cha asubuhi kwa kutoa wito kwa washiriki wote wa kanisa kuwa tayari kukubaliana na matokeo ya kura, alisisitiza kwa wote kwamba maamuzi yatakayotolewa na Mkutano Mkuu kubaki ndyo maamuzi ya juu kimamlaka katika kanisa la wa Sabato.

Ryan alihakikisha mkutano unaenda vizuri ilifuatiwa, Wajumbe walikubaliana mapema kujiepusha na makofi katika jitihada za kuweka hisia chini ya udhibiti.

Ryan, ambaye alitangaza matokeo ya mwisho ya kupiga kura, kwa uzito alishauri umati wa waliohudhuria katika ukumbi wa Alamodome ambao ulijikuta kupiga makofi mara baada ya matokeo, kwa kusema, "Hakuna kitu ushindi juu ya jambo hilo," alisema. "Hakuna washindi wala walioshindwa."

Erton Köhler, Rais wa Divisheni ya Amerika ya kusini aliunga mkono kauli ya Ryan kwa kusema haya hayakuwa mashindano ya kisiasa.
"Matarajio yangu kwa kanisa sio kuwa na washindi na walioshindwa, ila kila mtu apokee kujisikia uamuzi ni wa  Mungu na aufanye kuwa ni wake mwenyewe,"
"Naomba kila mtu awe na unyenyekevu kukiri kuwa Mungu anaweza kudhihirisha mapenzi yake kwa njia ambayo hutofautiana na mtizamo binafsi wa binadamu."

Jerry Page, Ministerial Association director, pia alisema. “Kama tukichukua muda katika maombi, kukiri kwa unyenyekevu, toba, na kuhudumia wengine, tunaweza kusonga mbele badala ya kuzunguka palepale au kurudi nyuma kwa sababu ya migogoro,”

“Sisi ni kanisa moja,” Ng alisema.

YESU anarudi upesi.!!!


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Toa maoni hapa...